Psalms 67

Mataifa Yahimizwa Kumsifu Mungu

Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za muziki. Zaburi. Wimbo.

1 aMungu aturehemu na kutubariki,
na kutuangazia nuru za uso wake,
2 bili njia zako zijulikane duniani,
wokovu wako katikati ya mataifa yote.

3 cEe Mungu, mataifa na wakusifu,
mataifa yote na wakusifu.
4 dMataifa yote wafurahi na kuimba kwa shangwe,
kwa kuwa unatawala watu kwa haki
na kuongoza mataifa ya dunia.
5 eEe Mungu, mataifa na wakusifu,
mataifa yote na wakusifu.

6 fNdipo nchi itatoa mazao yake,
naye Mungu, Mungu wetu, atatubariki.
7 gMungu atatubariki
na miisho yote ya dunia itamcha yeye.
Copyright information for SwhNEN